Kukadiria namba (Hisabati)

Hebu fanya kadirio la chini!
41 ni 40, 44 ni 40, 45 pia ni 40, 49 ni 40.
Inaitwa kukadiria chini nafasi ya kwanza.
?44/10 4
Kwa kuwa ni ukokotozi wa namba kamili, kama utagawanya kwa 10, itakuwa 4 badala ya 4.4.
?44/10*10 40
Gawanya kwa 10, na zidisha kwa 10, imemaliza kadirio la chini!
Hebu tufanye kadirio la juu!
49 ni 50, 45 ni 50, 44 & 41 pia ni 50, 40 ni 40.
Inaitwa kukadiria juu nafasi ya kwanza.
?44/10*10+10 50
Baada ya kukadiria chini, unaweza kuikadiria juu kwa kujumlishia 10!.
?40/10*10+10 50
Oh safi, 40 imebadilika na kuwa 50. Hebu amua kwa nafasi ya kwanza "ones place".
10 INPUT N 20 LET M,N%10 30 ?M
"%" ni alama ya kukokotoa baki katika ulimwengu wa IchigoJam BASIC.
Kama nafasi ya kwanza ni 0, ikadirie chini, na kama ni 1 au zaidi ikadirie juu.
40 IF M=0 ?N/10*10 50 IF M>=1 ?N/10*10+10
Jaribu sasa!
1. Hebu kadiria juu nafasi ya kwanza ya 72 kwa kutumia programu.
2. Hebu tengeneza programu ya "kukadiria namba" ambayo itakadiria chini nafasi ya kwanza kama ni 4 au chini yake na ikadirie juu kama ni 5 au zaidi yake.
3. Hebu tuhakiki kama inaweza kukadiria juu nafasi ya kwanza hata kwa "?(N+9)/10*10".
4. Hebu tengeneza programu ya kukadiria namba nafasi ya kwanza.
CC BY IchigoJam print https://ichigojam.github.io/print/sw/ IchigoJam®jig.jp